Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 18

Mithali 18:3-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
4Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
5Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
6Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
7Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
8Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
9Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
10Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
11Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
12Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
13Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
14Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
15Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.

Read Mithali 18Mithali 18
Compare Mithali 18:3-15Mithali 18:3-15