Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 17

Mithali 17:2-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
3Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
4Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
5Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
6Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
7Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
8Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
9Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
10Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
11Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.

Read Mithali 17Mithali 17
Compare Mithali 17:2-11Mithali 17:2-11