Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 17

Mithali 17:15-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
16Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
17Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
18Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
19Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
20Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
21Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
22Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.

Read Mithali 17Mithali 17
Compare Mithali 17:15-23Mithali 17:15-23