Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 15

Mithali 15:3-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
4Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
5Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
6Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
7Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
8Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
9Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
10Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
11Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu?
12Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.

Read Mithali 15Mithali 15
Compare Mithali 15:3-12Mithali 15:3-12