Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 15

Mithali 15:25-31

Help us?
Click on verse(s) to share them!
25Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
26Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
27Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
28Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
29Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
30Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
31Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.

Read Mithali 15Mithali 15
Compare Mithali 15:25-31Mithali 15:25-31