Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 13

Mithali 13:17-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
17Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.

Read Mithali 13Mithali 13
Compare Mithali 13:17-21Mithali 13:17-21