Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 13

Mithali 13:16-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
16Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.

Read Mithali 13Mithali 13
Compare Mithali 13:16-25Mithali 13:16-25