Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 13

Mithali 13:12-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.

Read Mithali 13Mithali 13
Compare Mithali 13:12-22Mithali 13:12-22