26Watu wanamlaani mtu ambaye hukataa kuuza nafaka, bali zawadi njema hufunika kichwa chake ambaye huuza nafaka.
27Yule ambaye hutafuta mema kwa bidii pia anatafuta kibali, bali yule atafutaye ubaya atapata ubaya.
28Wale wanaotumaini utajiri wataanguka, bali kama jani, wale watendao haki watasitawi.
29Yule ambaye analeta taabu kwenye kaya yake ataurithi upepo na mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye moyo wa hekima.
30Wale watendao haki watakuwa kama mti wa uzima, lakini vurugu huondoa uzima.