Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 11

Mithali 11:1-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Yehova huchukia vipimo ambavyo havipo sahihi, bali hufurahia uzani dhahiri.
2Kinapokuja kiburi, ndipo aibu huja, bali unyenyekevu huleta hekima.
3Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali udanganyifu wa njia za wajanja utawaangamiza.
4Utajiri hauna thamani siku ya ghadhabu, bali kwa kutenda haki hujilinda na mauti.
5Mwenendo wa mtu mwema huinyosha njia yake, bali waovu wataanguka kwa sababu ya uovu wao.
6Mwenendo mwema wa wale wampendezao Mungu utawalinda salama, bali wadanganyifu hunaswa katika shauku zao.
7Mtu mwovu anapokufa, tumaini lake hupotea na tumaini lililokuwa katika nguvu zake linakuwa si kitu.
8Yule atendaye haki hulindwa katika taabu na badala yake taabu humjia mwovu.
9Kwa kinywa chake asiyeamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa wale watendao haki hulindwa salama.

Read Mithali 11Mithali 11
Compare Mithali 11:1-9Mithali 11:1-9