Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 10

Mithali 10:9-17

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.

Read Mithali 10Mithali 10
Compare Mithali 10:9-17Mithali 10:9-17