Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 10

Mithali 10:2-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.

Read Mithali 10Mithali 10
Compare Mithali 10:2-16Mithali 10:2-16