Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 10

Mithali 10:13-27

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.

Read Mithali 10Mithali 10
Compare Mithali 10:13-27Mithali 10:13-27