Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mhubiri - Mhubiri 7

Mhubiri 7:12-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Kwa kuwa hekima hutoa ulinzi kama vile fedha inavyoweza kutoa ulinzi, lakini faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai kwa yeyote aliye nayo.
13Tafakaria matendo ya Mungu: Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?
14Wakati nyakati vinakuwa njema, ishi kwa furaha katika hali hiyo, lakini wakati unapokuwa mbaya, tafakari hili: Mungu ameruhusu hali zote ziwepo, Kwa sababu hii, hakuna mwanadamu yeyote atakaye fahamu chochote kinacho kuja baada yake.
15Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
16Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
17Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
18Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
19Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
20Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
21Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.

Read Mhubiri 7Mhubiri 7
Compare Mhubiri 7:12-21Mhubiri 7:12-21