Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mhubiri - Mhubiri 1

Mhubiri 1:2-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Mwalimu asema hivi, “Kama mvuke wa ukungu, kama upepo mwanana katika upepo, kila kitu hutoweka na kuacha maswali mengi.
3Ni faida gani wanadamu huipata kutoka katika kazi zote wazifanyazo chini ya jua?
4Kizazi kimoja huenda, na kizazi kingine huja, lakini nchi yabaki milele.
5Jua huchomoza na jua huzama na kwenda kwa kasi, na kurudi mahali linapochomozea tena.
6Upepo huvuma kusini na huzunguka kasikazi, na mara zote ukizunguka katika njia yake na kurudi tena.
7Mito yote hutiririka katika bahari, lakini bahari haijai. Mahali mito inakoenda, ndiko inakoenda tena.
8Kila kitu huwa uchovu, na hakuna yeyote awezae kukielezea. Jicho halishibina kile linachokiona, wala sikio halishibi na kile linachosikia.
9Chochote kilichopo ndicho kitakachokuwepo, kila kilichofanyika ndicho kitakachofanyika. Hakuna jipya chini ya jua.

Read Mhubiri 1Mhubiri 1
Compare Mhubiri 1:2-9Mhubiri 1:2-9