Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Matendo ya Mitume - Matendo ya Mitume 8

Matendo ya Mitume 8:4-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4waaminio ambao walikuwa wametawanyika bado walilihubiri neno.
5Filipo akashuka katika mji wa Samaria na akamtangaza Kristo huko.
6Baada ya makutano kusikia na kuona ishara alizofanya Filipo; wakaweka umakini juu ya kile alichosema.
7Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa, na wengi waliopooza na viwete waliponywa.
8Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.
9Lakini palikuwa na mtu mmoja katika mji ule jina lake Simon, ambaye alikuwa akifanya uchawi; ambao aliutumia kuwashangaza watu wa taifa la Samaria, wakati akisema kuwa yeye ni mtu wa muhimu.
10Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa, wakamsikiliza; wakasema;” mtu huyu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni kuu.”
11Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mrefu kwa uchawi wake.

Read Matendo ya Mitume 8Matendo ya Mitume 8
Compare Matendo ya Mitume 8:4-11Matendo ya Mitume 8:4-11