44Wote walioamini walikuwa pamoja na kuwa na vitu vyao kwa pamoja,
45na waliuza vitu na milki zao na kugawanya kwa wote kulingana na hitaji la kila mmoja.
46Hivyo siku baada ya siku waliendelea wakiwa na lengo moja katika hekalu, na walimega mkate kwenye kaya, na walishiriki chakula kwa furaha na unyenyekevu wa moyo;
47walimsifu Mungu na wakiwa na kibali na watu wote. Bwana aliwaongeza siku kwa siku ambao walikuwa wakiokolewa.