Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Matendo ya Mitume - Matendo ya Mitume 15

Matendo ya Mitume 15:25-35

Help us?
Click on verse(s) to share them!
25Kwa hiyo imeonekana vyema kwetu sote kuchagua watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,
26watu walio hatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana Yesu Kristo.
27Kwa hiyo tumemtuma Yuda na Sila, watawaambia mambo yayo hayo.
28Kwa kuwa ilionekana vyema kwa Roho Mtakatifu na kwetu, kutoweka juu yenu mzigo mkubwa kuliko mambo haya yaliyo ya lazima:
29kwamba mgeuke kutoka kwenye vitu vitolewavyo kwa sanamu, damu, vitu vya kunyongwa, na uasherati. Kama mtajiweka mbali na hivi, itakuwa vyema kwenu. Kwa herini.”
30Hivyo basi, walivyotawanyishwa, waliteremkia Antiokia; baada ya kukusanya kusanyiko pamoja, waliwasilisha barua.
31Walipokua wameisoma, walifurahi kwa sababu ya kutiwa moyo.
32Yuda na Sila, na manabii, waliwatia moyo ndugu kwa maneno mengi na kuwatia nguvu.
33Baada ya kukaa muda fulani huko, walitawanyishwa kwa amani kutoka kwa ndugu kwa wale waliowatuma.
34Lakini ilionekana vyema Sila kubaki huko
35Lakini Paulo na wengine walikaa Antiokia pamoja na wengine wengi, ambapo walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.

Read Matendo ya Mitume 15Matendo ya Mitume 15
Compare Matendo ya Mitume 15:25-35Matendo ya Mitume 15:25-35