Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Matendo - Matendo 15

Matendo 15:5-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, “Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata Sheria ya Mose.”
6Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalum wa kuchunguza jambo hilo.
7Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama, akasema, “Ndugu zangu, ninyi mnafahamu kwamba hapo awali Mungu alipenda kunichagua mimi miongoni mwenu niihubiri Habari Njema, ili watu wa mataifa wapate kusikia na kuamini.
8Naye Mungu anayejua mioyo ya watu, alithibitisha kwamba amewakubali kwa kuwapa nao Roho Mtakatifu kama alivyotupa sisi.
9Hakufanya ubaguzi wowote kati yetu na wao; aliitakasa mioyo yao kwa imani.
10Sasa basi, kwa nini kumjaribu Mungu kwa kuwatwika hao waumini mzigo ambao wala babu zetu, wala sisi hatukuweza kuubeba?
11Isiwe hivyo, ila tunaamini kwamba, sisi kama vile wao, tunaokolewa kwa njia ya neema ya Bwana Yesu.”

Read Matendo 15Matendo 15
Compare Matendo 15:5-11Matendo 15:5-11