Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Matendo - Matendo 15

Matendo 15:13-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Walipomaliza kuongea, Yakobo alianza kusema: “Ndugu zangu, nisikilizeni!
14Simoni ameeleza jinsi Mungu hapo awali alivyojishughulisha na watu wa mataifa mengine, akachagua baadhi yao wawe watu wake.
15Jambo hili ni sawa kabisa na maneno ya manabii, kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
16Baada ya mambo haya nitarudi. Nitaijenga tena ile nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitayatengeneza magofu yake na kuijenga tena.
17Hapo watu wengine wote, watu wa mataifa yote niliowaita wawe wangu, watamtafuta Bwana.
18Ndivyo asemavyo Bwana, aliyefanya jambo hili lijulikane tangu kale.

Read Matendo 15Matendo 15
Compare Matendo 15:13-18Matendo 15:13-18