Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Matendo - Matendo 14

Matendo 14:13-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Naye kuhani wa hekalu la Zeu lililokuwa nje ya mji akaleta fahali na shada za maua mbele ya mlango mkuu wa mji, na pamoja na ule umati wa watu akataka kuwatambikia mitume.
14Barnaba na Paulo walipopata habari hiyo waliyararua mavazi yao na kukimbilia katika lile kundi la watu wakisema kwa sauti kubwa:
15“Ndugu, kwa nini mnafanya mambo hayo? Sisi pia ni binadamu kama ninyi. Na, tuko hapa kuwahubirieni Habari Njema, mpate kuziacha hizi sanamu tupu, mkamgeukie Mungu aliye hai, Mungu aliyeumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo.
16Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda.
17Hata hivyo, Mungu hakuacha kujidhihirisha kwa mambo mema anayowatendea: huwanyeshea mvua toka angani, huwapa mavuno kwa wakati wake, huwapa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”
18Ingawa walisema hivyo haikuwa rahisi kuwazuia wale watu wasiwatambikie.

Read Matendo 14Matendo 14
Compare Matendo 14:13-18Matendo 14:13-18