Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Matendo - Matendo 11

Matendo 11:22-26

Help us?
Click on verse(s) to share them!
22Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.

Read Matendo 11Matendo 11
Compare Matendo 11:22-26Matendo 11:22-26