Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Matendo - Matendo 10

Matendo 10:11-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
11Aliona mbingu zimefunguliwa na kitu kama shuka kubwa inateremshwa chini ikiwa imeshikwa pembe zake nne.
12Ndani ya shuka hiyo kulikuwa na kila aina ya wanyama: wanyama wenye miguu minne, wanyama watambaao na ndege wa angani.
13Akasikia sauti ikimwambia: “Petro, amka uchinje, ule!”
14Petro akajibu, “La, Bwana; mimi sijaonja kamwe chochote ambacho ni najisi au kichafu.”
15Ile sauti ikasikika tena ikimwambia: “Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa!”
16Jambo hili lilifanyika mara tatu, kisha ile shuka ikarudishwa juu mbinguni.
17Petro alipokuwa bado anashangaa juu ya maana ya hilo maono alilokuwa ameliona, wale watu waliotumwa na Kornelio, baada ya kuigundua nyumba ya Simoni, walifika mlangoni,
18Wakaita kwa sauti: “Je, kuna mgeni humu aitwaye Simoni Petro?”

Read Matendo 10Matendo 10
Compare Matendo 10:11-18Matendo 10:11-18