Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Marko - Marko 8

Marko 8:6-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
6Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
7Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
8Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
9Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
10Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
11Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
12Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
13Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
14Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
15Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
16Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”

Read Marko 8Marko 8
Compare Marko 8:6-16Marko 8:6-16