Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 6

Luka 6:21-31

Help us?
Click on verse(s) to share them!
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.

Read Luka 6Luka 6
Compare Luka 6:21-31Luka 6:21-31