Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 2

Luka 2:1-6

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,

Read Luka 2Luka 2
Compare Luka 2:1-6Luka 2:1-6