Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 23

Luka 23:40-48

Help us?
Click on verse(s) to share them!
40Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
41Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
42Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
43Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
44Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
45Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
46Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
47Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
48Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.

Read Luka 23Luka 23
Compare Luka 23:40-48Luka 23:40-48