Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 1

Luka 1:49-72

Help us?
Click on verse(s) to share them!
49Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.”
56Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale.
71Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:49-72Luka 1:49-72