Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 1

Luka 1:40-55

Help us?
Click on verse(s) to share them!
40Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46Naye Maria akasema,
47“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.”

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:40-55Luka 1:40-55