Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Luka - Luka 1

Luka 1:33-40

Help us?
Click on verse(s) to share them!
33Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho.
34Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:33-40Luka 1:33-40