Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 1

Luka 1:12-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.

Read Luka 1Luka 1
Compare Luka 1:12-16Luka 1:12-16