Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Luka - Luka 14

Luka 14:14-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
14nawe utakuwa umepata baraka, kwa kuwa hao hawana cha kukulipa. Maana Mungu atakupa tuzo lako wakati watu wema watakapofufuka.”
15Mmoja wa wale waliokuwa wameketi pamoja na Yesu akasema, “Ana heri mtu yule atakayekula chakula katika Ufalme wa Mungu.”
16Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alifanya karamu kubwa, akaalika watu wengi.
17Wakati wa karamu ulipofika alimtuma mtumishi wake awaambie walioalikwa, Njoni, kila kitu ni tayari.
18Lakini wote, kwa namna moja, wakaanza kuomba radhi. Wa kwanza akamwambia mtumishi: Nimenunua shamba, kwa hiyo sina budi kwenda kuliangalia; nakuomba uniwie radhi.

Read Luka 14Luka 14
Compare Luka 14:14-18Luka 14:14-18