Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 25

Hesabu 25:5-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
6Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
7Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
8Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
9Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
10BWANA akanena na Musa, akasema,
11“Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
12Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.

Read Hesabu 25Hesabu 25
Compare Hesabu 25:5-12Hesabu 25:5-12