Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Hesabu - Hesabu 10

Hesabu 10:12-24

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
13Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
14Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
15Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
16Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
17Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
18Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
19Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
20Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
21Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
22Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
23Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
24Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.

Read Hesabu 10Hesabu 10
Compare Hesabu 10:12-24Hesabu 10:12-24